Kesi ya ulipuaji bomu iliyoteguliwa yaweka uhusiano baina ya Kenya na Iran mashakani | Gossip Wire
Breaking News
Loading...

Friday, May 24, 2013

Kesi ya ulipuaji bomu iliyoteguliwa yaweka uhusiano baina ya Kenya na Iran mashakani

Na Julius Kithuure, Nairobi
Tangu mahakama ya Kenya ilipotoa hukumu kwa raia wawili wa Iran kwenda jela kifungo cha maisha kutokana na mashtaka yanayohusiana na ugaidi mapema mwezi huu, hali ya baadaye ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Nairobi na Tehran imekuwa wa mashaka, kukiwa na uwezekano wa kurudisha nyuma matumaini ya Iran ya kupanua shughuli na uwepo wake kisiasa nchini Kenya kwa miaka ijayo.
Sayed Mansour (katikati) na Ahmad Mohammed (kulia), wote wawili ambao ni raia wa Iran, wanafungwa pingu mara tu baada ya kuhukumiwa kifungo cha maisha jela hapo tarehe 6 Mei kutokana na mashtaka yanayohusiana na ugaidi, ikiwa ni pamoja na kumiliki iliyodaiwa kuwa milipuko kwa ajili ya kutumia katika mashambulio ya bomu. [Simon Maina/AFP] Sayed Mansour (katikati) na Ahmad Mohammed (kulia), wote wawili ambao ni raia wa Iran, wanafungwa pingu mara tu baada ya kuhukumiwa kifungo cha maisha jela hapo tarehe 6 Mei kutokana na mashtaka yanayohusiana na ugaidi, ikiwa ni pamoja na kumiliki iliyodaiwa kuwa milipuko kwa ajili ya kutumia katika mashambulio ya bomu. [Simon Maina/AFP]
Mgogoro huo wa kidiplomaisa ulitokana na shambulio la ugaidi lililoteguliwa nchini Kenya ambalo lililotolewa hukumu na mahakama ambalo lilikuwa limepangwa na Ahmed Mohammed, mwenye umri wa miaka 50, na Sayed Mansour, mwenye umri wa miaka 51, wote wawili raia wa Iran. Wanaume hao wawili walikamatwa mwezi Juni mwaka uliopita nje ya Laico Regency, hoteli yenye nyota tano inayomilikiwa na Mlibiya katikati ya Nairobi, siku nane baada uchunguzi mkubwa uliofanywa na Kitengo cha Polisi Kinachopambana na Ugaidi.
Tarehe 2 Mei, walitiwa hatiani kwa kumiliki kilogramu 15 za milipuko yenye nguvu ya RDX, ambayo polisi waligundua kufukiwa kwenye uwanja wa gofu. Mahakama ya Nairobi ilisema Mohammed na Mansour walishukiwa kuhusika na ulipuaji bomu uliopangwa na mtandao wa kigaidi huko Mombasa na Nairobi. Wanaume wote hao wawili walikana mashtaka hayo.
Lakini polisi wa Kenya walitetea uamuzi wao wa kuwakamata na kuwafungulia mashtaka Wairani hao wawili.
Msemaji wa polisi Charles Owino aliiambia Sabahi kwamba polisi hawakuwawekea wanaume hao, wala maofisa waliowakamata walifanya hivo kutokana na maelekezo kutoka kwa serikali yoyote ya nje wakati walipowafunga.
"Polisi wa Kenya walifanya uchunguzi wa kina kuhusu wanaume hao wawili, hivyo kuzuia uhalifu mkubwa wa kigaidi kutokutokea katika nchi," Owino alisema. "Nina furaha kwamba tulitahadharishwa na kwamba mwishowe tuliendesha mashtaka kwa mafanikio."
Baada ya Mohammed na Mansour kuhukumiwa kwenda jela maisha tarehe 6 Mei, vyombo vya habari vya ndani na vya kimataifa viliripoti kuwa Wairani hao wawili walikuwa wakifanya kazi na kikosi maalum cha Quds, kitengo cha siri cha kikundi cha Ulinzi cha Mapinduzi ya Kiislamu cha Iran ambacho hufanya operesheni nje ya nchi.
Balozi wa Iran nchini Kenya Malik Hussein Givzad alikana madai hayo, akisema wanaume hao wawili wa nchini kwake walikuwa watalii nchini Kenya wakiwa na viza halali.
Kutoka siku ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Givzad aliiambaia gazeti la Daily Nation la Kenya kwamba Iran ina uhusiano mzuri wa kibiashara na Kenya na kwamba kutiwa hatiani kwa Mohammed na Mansour kusingesababisha kuvunjwa kwa uhusiano wa kidiplomasia.
"Huu ni mchakato wa mahakama, ambao tunauheshimu," Givzad alisema, akiongezea kwamba Iran itawasaidia wanaume hao wawili kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

'Kenya inapaswa kutaka majibu'

Sio kila mmoja ana matarajio mazuri kuhusu kuhusu siku zijazo za uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Iran.
"Serikali ya rais Uhuru Kenyatta inapaswa kuwa jasiri na kukata uhusiano huu wa hatari wa kidiplomasia na Tehran kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba Wairani waliokamatwa ni mawakala wa siri wa Walinzi wa Jamhuri ya Iran, kama ambavyo Polisi wa Kuzuia Ugaidi na Intelijensia ya Usalama wa Taifa wamekuwa wakidai," alisema Ignacious Kamau Njoroge, ofisa usalama aliyestaafu, mwenye miaka 67 katika jeshi la Kenya na mkurugenzi wa shirika la upelelezi la Global Eye Spies & General Investigations iliyo na makao mjini Nairobi.
Njoroge alisema Kenya inapaswa kumrejesha balozi wake huko Iran na kutuma barua ya malalamiko kwa serikali ya Iran na Umoja wa Mataifa kwa sababu ya ukubwa wa tuhuma na majanga ambayo ingetokea iwapo mlipuko huo ungefanyika.
"Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya inapaswa kuacha njia zake za sasa na msimamo wa 'biashara kama kawaida' na kumuita kwa haraka balozi wa Iran nchini Kenya na kumuagiza aelezee anachokijua kuhusu mashtaka ya pande zote mbili badala ya balozi kutoa taarifa zisizoshawishi na kutoa maelezo ya kukiri kosa katika mkutano na vyombo vya habari," Njoroge aliiambia Sabahi.
"Na, sababu Wairani walioshitakiwa dhahiri walipinga kushirikiana na waendesha mashtaka na wanaowahoji wa Kenya kama mwendesha mashtaka alivyoeleza mahakamani, Kenya inapaswa kutaka majibu kutoka Iran, vinginevyo tutahitimisha kwamba hawa wawili waliapa faragha na serikali zao ili kubaki kimya kutunza utambulisho wao na matakwa ya nchi yao," alisema Njoroge.
Serikali ya Kenya inapaswa pia kutazama jinsi takriban kilogramu 15 za vifaa vya ulipuaji vilivyoingia nchini bila kutambulika, alisema Njoroge.
"Serikali inapaswa kuchunguza kwa kina kutoka katika serikali ya Iran jinsi nchi hizi mbili zilivyopata vifaa vya kutengenezea mabomu, hati zao za utambulisho hasa ni zipi na ni wapi walikuwa wakilenga," alisema.

Kenya sio uwanja wa michezo kwa 'misheni za kulipiza kisasi za Iran'

Robert Kamau, mhadhiri wa uhusiano wa kimataifa na diplomasia katika Chuo Kikuu cha Nairobi, alisema Kenyatta anapaswa kukamata fursa hii wakati jumuiya ya kimataifa ikifuatilia.
"Rais Kenyatta, anayejaribu kushinda upendeleo wa jumuiya ya kimataifa na ushirikiano baada ya mashtaka yake ya Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), anapaswa kukamata fursa sasa hivi na kutoa ujumbe mkali kwamba Iran ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa ulimwengu na kwamba Kenya inapaswa kutofumbia macho vitendo hivyo katika himaya yake," aliiambia Sabahi. "Hii ndiyo sababu hasa [Kenya] ilijitolea wanajeshi wake na rasilimali kupigana na al-Shabaab kwa kina nchini Somalia."
"Nina uhakika kuwepo kwa Wairani na shughuli nchini Kenya zinakwenda zaidi ya nyanja halali za kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni," alisema Kamau. "Kwa hakika Irani na shirika lake la usalama wanashughulikia kwa siri ugaidi na uchochezi, ili kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Israeli na Marekani, nchi hizo kuu mbili ambayo inazichukia."
"Lakini Kenya, kama nchi inayopenda amani na inapaswa kuakataa kuwa uwanja wa michezo kwa ajili ya misheni ya ulipizaji kisasi wa Iran nje ya nchi," alisema.
Njoroge alisema mkutano unaofaa wa kipelelezi una uwezekano wa kuonyesha kwamba shambulio lililokusudiwa kuhusu Kenya linaoana kwa mtindo wa kiharamia wa Kiirani. Tarehe 13 Februari, 2012, walipuaji wa Iran walimvamia mtumishi wa ubalozi wa Israeli katika mji mikuu ya India na Georgia, na siku moja baadaye walipanga kufanya mashambulio kama hayo huko Thailand na Azerbaijan lakini walikwamishwa. Kama sehemu ya kiwango chao cha utaratibu wa kufanya kazi, serikali hiyo ilikanusha vikali kuhusika na mashambulio hayo pia, alisema Njoroge.
Simiyu Werunga, ofisa jeshi mtaafu wa Kenya na Mkurugenzi mkuu wa Kituo cha Afrika kwa ajili ya Usalama na Stadi za Kimkakati, alisema hakuna yeyote aliyetarajia kwamba serikali ya Iran itajitokeza hadharani na kukiri kutuma wakala wa ulipuaji bomu nchini Kenya.
"Kikosi cha Polisi cha Kenya [Kitengo] na wakala wa upelelezi wa kitaifa, Shirika la Upelelezi la Taifa, vinapaswa kumpa taarifa rais ipasavyo pamoja na taarifa sahihi za kipelelezi kuhusu uhusika wao katika kesi hii ili mkuu wa nchi atoe agizo la uamuzi wa hatua za kidiplomasia kuhusu upelelezi thabiti," Werunga alisema.

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT