KENYA:Machafuko ya Delta ya Mto Tana yalisababishwa na mzozo juu ya rasilimali, tume ya uchunguzi yasema | Gossip Wire
Breaking News
Loading...

Friday, May 24, 2013

KENYA:Machafuko ya Delta ya Mto Tana yalisababishwa na mzozo juu ya rasilimali, tume ya uchunguzi yasema

Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokana na "mzozo wa rasilimali", Tume ya Mahakama ya Uchunguzi iliyopewa kazi ya kuchunguza mauaji hayo ilihitimisha katika ripoti yake iliyowasilishwa kwa Raisi Uhuru Kenyatta Jumatano (tarehe 22 Mei).
Hakimu Bi. Grace Nzioka aliwasilisha ripoti kwa Kenyatta miezi saba baada ya tarehe ya awali iliyokuwa itolewe mwezi Oktoba. Kenyatta aliahidi kupitia mambo yaliyogunduliwa na tume na "kuchukua hatua zinazofaa," kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya habari ya Raisi.
Matokeo yanaondoa shutuma za awali kwa Inspekta Mkuu wa Polisi David Kimaiyo na wengine kwamba vurugu huko Mto Tana ilikuwa iliyochochewa na wanasiasa.
Aliyekuwa Msaidizi wa Waziri Dhadho Godhana aliondolewa kutoka wadhifa wake baada ya kushutumiwa kuhusika katika mapambano hayo. Baadaye aliachiliwa na Mahakama Kuu.

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT