TANZANIA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA | Gossip Wire
Breaking News
Loading...

Tuesday, March 25, 2014

TANZANIA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA



Na Faraja Simon
Tuwe makini na wanasiasa na tusiwaamini hata chembe hasahasa kwa hili la wao Kuhodhi mchakato wa uandishi wa katiba mpya.

Siasa ni sehemu ya maisha ya kila mtanzania hatuwezi kujitenga na siasa au siasa kutengwa nasi kwani imebeba mustakabali wa taifa letu.Pamoja na kuwa katiba ni political document , tuwe makini na siasa kuhodhi mchakato mzima wa bunge la katiba.Tusiruhusu wanasiasa kutufanyia maamuzi kwa madai kwamba ndio maamuzi ya watanzania zaidi ya milioni 44.Sio Madai na hoja zote za wanasiasa ni madai ya wananchi.N sio kweli kwamba wengi wao watasimamia na kutetea hoja za wananchi.

Wanasiasa watatafuta afueni ya vyama vyao hapo badae.Watawala wanatafuta katiba itakayotoa mwanya wa wao kuendelea kushika dola na wapinzania wanataka katiba itakayo wapa mwanya wa wao kushika dola kirahisi.Wanasiasa watatetea ugali wa watoto wao na nafasi zao hapo badae. Wengine wanatafuta ahuheni ya nafasi zao na za makundi yao hapo baadaye.Kwa hivyo ni wachache sana wanaofanya maamuzi yao kitaifa pasi na chembe za uchama.

Tusisahau kuwa uzalendo kwa wanasiasa wetu si wa kuridhisha, namaanisha ubinafsi umetawala fikra zaoWengi wao ni wachumia tumbo ,tusipokuwa makini watatuharibia katiba yetu kwa kuandika katiba yenye misingi na matakwa yao.Pamoja na kwamba tuna nafasi ya kuipigia kura ila tusisahau wanasiasa wana sauti ya kuwaaminisha watanzania visivyo vya kweli na kwa kuwaamini, tukawafuata.Hii itakuwa hatari kubwa kwa taifa letu.


Hatuna budi kuijenga,kuilinda na kuitetea Tanzania tunayoitaka. Ni Tanzania thabiti na yenye nguvu kubwa kiuchumi, kiusalama, siasa safi zenye lengo la kumkomboa mwananchi pale tu uzalendo utakapotunzwa kama lulu katika mioyo ya watanzania, pale rushwa atakapokuwa adui wa kila mtanzania, na Pale viongozi wa taifa hili watakapozika ubinafsi na kuishi uzalendo, kutetea rasilimali za taifa kwa manufaa ya taifa hili, wakiongoza mgawanyo sawa wa matunda ya rasilimali kwa taifa.


Tanzania inahitaji mabadiliko katika Nyanja zote.Hatuwezi kukataa mabadiliko au kuyapinga, tutayachelewesha tu.Tanzania inahitaji viongozi watendaji na sio waongeaji,watakaothubutu kuwa chachu ya mabadiliko chanya katika nyanja zote za maisha ya Mtanzania. Viongozi wenye maamuzi ya kizalendo kwa manufaa ya watanzania.Maamuzi wanayoyafanya au waliyowahi kuyafanya viongozi wetu kwa maslahi yao binafsi au ya mrengo wao yamelitafuna taifa na kuliweka hapa lilipo, yamepoteza dira ya Tanzania kama taifa.


Naamini Tanzania tunayoitaka ipo na itakuwa.Vijana tunaweza kuweka pembeni itikadi za kisiasa na kidini, ukabila, na ubinafsi.Na kuuvaa uzalendo na spirit ya kufanya kazi kwa bidii,kuichukia rushwa kwa moyo wetu wote,  kuwa watendaji zaidi ya waongeaji kwa manufaa ya Tanzania yetu. Tusiseme "walikula sasa zamu yetu".Bali tupatapo nafasi twende tukafanye kazi ya kuwatumikia watanzania kwa uaminifu na uzalendo wa hali ya juu.Tuwe na fikra za mabadiliko kwani naamini ipo siku vijana tutaandika historia mpya kwa taifa hili.


Na Faraja simon

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT