Gossip Wire: KALAMU YA FARAJA
Breaking News
Loading...
Showing posts with label KALAMU YA FARAJA. Show all posts
Showing posts with label KALAMU YA FARAJA. Show all posts

Sunday, May 11, 2014

AFRIKA TUNA CHA KUJIFUNZA KWA UONGOZI WA RAIS KENYATTA NA JUHUDI ZAKE ZA KUIKOMBOA AFRIKA KIUCHUMI.

Na Faraja Simon
Pongezi zangu kwa rais wa Kenya kwa kuonyesha uwazi hasa kwa kuweka mkataba waliokubaliana na serikali ya uchina wazi. Sio kitu rahisi hata kidogo kwa mataifa ya afrika kufanya kitendo hicho. Ameweka wazi kupitia ukurasa wake wa facebook. kuisoma fuata link hii UHURU KENYATTA.



Kijana huyu amekuwa mstari wa mbele kutetea na kuonyesha nja kwa afrika kukuza pato la ndani kwa kufungua milango ya biashara kati ya nchi moja ya afrika kwenda nyingine.Hapa juzi kwenye world economic forum alikuwa na ajenda hiyohiyo ya kuongeza masoko ya ndani na free movement of goods.Kuwapa nafasi wawekezaji wa ndani kuwekeza ndani ya Afrika. Kuondoa vizuizi vya kibiashara na mengineyo.Haya ni maneno yake aliyoandika may 7 2014 kupitia ukurasa wake wa Facebook:
"Today during the World Economic Forum onAfrica, I called on all African leaders to work together in removing obstacles that hinder movement across the continent. Free movement of people, goods and services will increase intra-Africa trade and help the continent achieve its development targets. Lack of political will and negative perception should not be allowed to undermine Africa’s integration and economic growth. As leaders, we should not block African investors from investing in the continent by imposing stiff regulations and cumbersome visa requirements. We need to facilitate our business people to trade within the continent more freely. There is no reason why we cannot begin by issuing proven African investors with visas allowing them to do their work with minimum of difficulties. We signed the call to action by the World Economic Forum’s Global Agenda Council on Travel and Tourism."

Kijana huyu ana kitu cha tofauti bado hakijaonekana ila naamini ipo siku kitaonekana. Afrika izidi kumpa nafasi na kummunga mkono katika kuikomboa Afrika kiuchumi.

Kaonyesha njia kwa wana Afrika na Afrika mashariki kwa ujumla na ni nafasi kwa Tanzania kujifunza kupitia hilo. Mh: JK mikataba mnayotia sahihi iwekeni wazi tuione. Mnaficha nini ingali taifa ni la watanzania tupeni nafasi ya kuona makubaliano yenu.

Najua unatangaza uwazi kwa serikali yako, ila mkuu wangu wa nchi jaribu kuwa muwazi kwenye serikali yako. Uwazi ni pamoja na mikataba hiyo kuwa wazi. Demokrasia ni pamoja na mikataba hiyo kuwa wazi. Embu angalia hili suala mkuu na jua lipo ndani ya uwezo wako.

-F.S

Tuesday, May 6, 2014

WARAKA WANGU KWA VIJANA WENZANGU KWA MWAKA 2014: MAISHA BORA YANAJENGWA NA WEWE M WENYEWE UKIAMUA.



Na. FARAJA SIMON
Maadamu tupo hai tunanafasi ya kuboresha maisha yetu. Tusiache kutumia fursa tulizonazo hata kama ni ndogo, kuboresha maisha yetu. Kila mtu ana matatizo na vizuizi vingi katia safari ya kuhakikisha tunakuwa na maisha bora.Ukweli ni kwamba hayo yote hayatufanyi kutofikia ndoto zetu.Matatizo yasitukatishe tamaa bali tuyachukulie kama changamoto katika kuboresha maisha yetu kisha tusonge mbele na kamwe tusirudi nyuma.

Bidii ya kazi ni muhimu sana,tuwe na moyo mkuu katika kufanya kazi kwa bidii huku tukijiwekea malengo mafupi na marefu kadiri muda utakavyoruhusu.Tusisahau muda si mali yetu,hivyo tusisubiri kesho wala badae ikiwa mungu katupa uzima.Tufanye kazi bila kudharau kazi kwani hakuna aliyeanza na mamilioni bali wote wameanzia chini.

Tuondoe  fikra kwamba kazi hii si hadhi yangu au ile ni hadhi yangu.Kazi haina hadhi ilimradi inaingiza kipato hata kama ni kidogo kwani si sawa na kukaa bure.Upatapo fursa ya kufuga kuku itumie na ipende nayo itakutoa.ikiwa umepata fursa ya kulima basi itumie ipasavyo na bila kukata tamaa, utayaona mafanikio.Sio lazima sote tukae katika ofisi zenye viyoyozi ndo ujione kuwa una kazi. Kijana kazana na chochote unachoweza kukifanya, usikate tamaa, chukua hatua nyingine mbele uweze kufikia lengo lako.

Ni vyema kutafuta elimu ya ujasiriamali ili tuweze kutawala fedha vyema na kutengeneza michanganuo ya biashara kwa ustadi mkubwa. Pia kufanya tafiti kwa waliopiga hatua kiuchumi. Hii itatusaidia kwenda na kasi ya dunia ya sasa.Pia itatufungua zaidi juu ya kuzitambua fursa zinazotunguka. Hii itaongeza ujasiri wa kuthubutu kwetu sisi vijana.Safari si ndefu sana, Reginald Mengi (kwa mfano) tutamfikia tu kwani hakuanza juu bali alianza chini kwenda juu.Vijana wenzangu wa kitanzania Tusikate tamaa kesho yetu imekwisha kufika.

Serikali bora, sikivu na mathubuti ni moja ya chachu muhimu katika maendeleo ya vijana.hivyo, shime, shime vijana tupatapo nafasi ya kufanya uchaguzi tuitumie kwa busara na hekima zilizotukuka kuchagua viongozi watakaotufungulia fursa za kuiona kesho yetu.Viongozi watakaoona ipo sababu ya kuwalinda vijana na kuwaongoza katika kujikwamua kiuchumi.tusichague kiongozi kwa sababu ya ushabiki wa kichama, kikanda, kikabila, kidini, kindugu wala kwa kufata mkumbo.baada ya kusikiliza sera zao  ni vyema tukafanya uchanganuzi binafsi na maamuzi binafsi juu ya mustakabali wa taifa letu na maisha yetu kwa kuchagua kiongozi bora na atakayetuongoza katika kuipeleka nchi yetu mahala bora zaidi.

Vijana wenzangu, Maisha bora yanajengwa na wewe mwenyewe ukiamua.Maisha bora yanaanzia kwako kwako.Weka nia, bidii, na jitihada za dhati pamoja na ujasiri wa kuthubutu katika kujijenga kiuchumi tutumie fursa zilizopo tukiuheshimu muda nasi tutaboresha maisha yetu.Kijana chukua hatua madhubuti kuweza kujikwamua kiuchumi.
 Imeandikwa na Faraja Simon
            Email: farajasimon@yahoo.comfarajasimonm@gmail.com
            mobile: +255787539392, +255763222443

Saturday, April 26, 2014

NILIWAHI KUANDIKA MAKALA HII HAPA OCTOBER 2013 JUU YA NGUVU KUBWA WANAYOTUMIA MATAIFA YA MAGHARIBI KUPITIA MWAMVULI WA ICC NA UHUSIANO WAO NA UKOLONI MAMBO LEO. TUJIKUMBUSHE HAYA:

AFRICA NA UKOLONI MAMBO LEO NA ICC: KWANINI AFRICA?
Maisha ya binadamu hayajawahi kuwa maraisi au mepesi. Kila mmoja hupambana ili kuweza kuyamudu. Kuna njia nyingi za kupambana ila moja kubwa inayotumiwa na mabepari (capitalist)  ni kunyonya mataifa dhaifu (maskini). Hutumika kila njia ikiwezekana kuhatarisha maisha ya maskini ili kujinufaisha. Utu kwa bepari ni nadharia tu. Kwani hutunga chochote kile kulinda nafsi yake (status) katika Dunia.
            Waliamua kuitawala Africa ili kuweza kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyao pamoja na soko la bidhaa zao kutokana na ushindani uliokuwepo. Hapa walikuja kama wamisionari, wafanyabiahsara na wanajiografia. Hayo yote yalikuwa ni mwamvuli tu. Bali lengo kuu ni unyonyaji wa nguvu kazi ya Africa na rasilimali za Africa.
            Waafrica wenzangu, tutambue ukoloni ulikufa na sasa wanatumia ukoloni mamboleo. Mimi huita scientific colonialism, hutumia uwezo wao wa sayansi na teknolojia katika kutimiza  adhima yao ya kuzitumia rasilimali za Africa na wanatumia njia zozote za kuvuna rasilimali hizi pasipo Africa kujielewa. Kuna njia nyingi ila moja ni kuwathibiti viongozi hawa wa Africa ambao wamekuwa wazalendo kwa Nchi zao na hawautaki ubeberu wao. Basi viongozi hawa hudhibitiwa kwa njia mbili:
            Moja ni kwa mapinduzi ya waasi, hili mataifa haya huwafadhili waasi kwa siri sana, ili kuziondoa serikali hatarishi uongozini wapate upenyo wa kuendeleza unyonyaji (Divide and rule).
            Pili ni hii mahakama ya ICC (The Hague). Hutumia mahakama hii kama fimbo ya kuwaadabisha viongozi wa kiafrica. Rais wa Libya asingekufa angekuwa the Hague, vivyovivyo kwa Misri, Sudan na sasa ni Kenya. Africa lazima tuungane katika hili kwani leo ni Kenya kesho Uganda, Tanzania, Malawi na hata Africa kusini pale tutakapokuwa ukuta kuzuia unyonyaji wao.
            Ndipo swali hili linakuja kwa nini Africa? Ni swali kila mzalendo wa Africa atajiuliza, kwa nini Afrika! Na sio Ulaya, Amerika, Australia na Asia? Je, umoja wa mataifa ni kwa ajili ya Afrika pekee?
            Ijumaa ya tarehe 10/10/2013 Nchi wanachama wa umoja wa Africa watakutana mjini Addis Ababa mada kuu ikiwa ni mahusiano ya Africa na ICC. Shukran kwa Kaguta Yoweri Museven. Suala hili linaumiza kichwa diplomasia ya Ulaya na America huku ikiwa kama panaweza kutokea shinikizo la Nchi wanachama wa umoja wa Africa kujitoa katika mkataba wa Rome.
            Waafrica wenzangu, ni lazima tujiulize maswali juu ya uwepo wa ICC na utendaji wake ndani ya Africa. Kwanini ni viongozi wa kiafrica tu ndio wanao kwenda The Hague? Je! Wanataka kutuambia kuwa mataifa  ya Magharibi hawakiuki haki za binadamu? Tujiulize kuhusu alichokifanya George W. Bush kule Iraq na Pakistan, walichokifanya umoja wa Ulaya na Marekani(Obama) kule Libya. Je, hii haitoshi kuwashitaki nao wakaenda The Hague? Kwa nini Afrika?
            Wafrika wenzangu, tumekuwa wanyonge sana na tumekosa umoja ya kusema sasa inatosha kwa udhalimu huu wa ICC. Tafadhali viongozi wan chi wanachama wa umoja wa Afrika mkutanapo tar 10/10/2013 muwe na sauti moja yenye maamuzi magumu itakayoitikisa Dunia na kuifikishia ujumbe kuwa udhalimu na unyonyaji huu umetosha, umefika kikomo
            Nionavyo ni vyema umoja wa Africa ukawa na mahakama yake ili kuweza kuyamaliza mambo ya ndani ya Africa, kwani tuna tamaduni zetu za kumaliza mizozo, na tuna tamaduni zetu za kusuluhishana. Haina haja ya ICC kuendeleza udhalimu huu Afrika. Tuungane pamoja katika maamuzi ya kujenga Africa madhubuti.
            Sio hivyo tu, bali najiuliza pia mahakama hii ilianzishwa kwa misingi gani? Nani walikuwa walengwa? Kuna nini nyuma ya mahakama hii? Tuangalie zaidi ya kikomo cha macho yetu yaonapo. Naamini kwa mwendo wa ICC, basi ni dhahiri kuwa ni fimbo ya kuiongoza Africa katika kuimarisha na kusimika mizizi ya ubepari Africa.
            Tumewahi kujiuliza ni nani anayewafadhili waasi Africa? Je ni kweli huitaji kuingia madarakani kwa demokrasia tena walioileta wao wenyewe ? wao wenyewe tena husaidia waasi kuingia madarakani? Ni dhahiri kuwa kuna tusichokiona hapa. Nani anayegharamikia silaha wanazotumia waasi?, ni nani aliyenyuma yao? Kwa mfano wa Libya, ni nani aliyewaandaa waasi katika kumwangusha simba wa Africa aliyekuwa adui mkubwa wa Amerika? Lazima  tukubali yaliyotokea Libya haikuwa ridhaa ya wanalibya bali kuna siri nzito nyuma yake. Kwanini Afrika?
            Waafrica wenzangu haya yote yanayofanyika na wabepari hatuyaoni? Kwa nini tuwahukumu waafrica wenzetu? Kwa nini tutumike kama chombo cha kuiangamiza Africa yetu kwa faida ya wabepari? Kwa nini tufanywe wajinga na wavivu wa kufikiri kiasi hicho. Tuseme imetosha, pamoja tujenge Africa mathubuti.
Mazingira ya machafuko ya kisiasa Afrika huziandaa wenyewe kwa agenda zao za siri kisha wanakuja kutuadhibu na chombo hichi, mahakama ya ICC.Nataka tuelewe kuwa mbali na mahakama hii viongozi wengi wa Africa huwekwa madarakani wakiwa wameandaliwa kutimiza matakwa ya mabepari. Viongozi wengi wa Africa ni mapandikizi ya mabepari yanayoiangamiza Africa yao wenyewe ndio maana hawana maamuzi ya umoja.
Funguka Africa, ICC ni kiini macho tu, kuna mengi nyuma ya pazia. Tuukatae ukoloni mamboleo ulioshika mizizi. Tuwe wamoja kujenga Africa mathubuti, tusipigane wenyewe kwa wenyewe, tukatae kuwa mashabiki wa magharibi. Tujifunze kwa Libya walivyoishabikia America, Nato na waasi pasipo kujua kuwa wanajiangamiza wenyewe. Je divide and rule haijatunga kazi kule Libya? Marekani alichukua tani ngapi za matuta? Fikiri kwa nini Afrika?
Waafrica wenzangu, tuache ushabiki wa kisiasa ulio na hisia za kipandikizi pasipo kujijua, tutaiangamiza Africa sisi wenyewe.Historia imetuweka tulipo lakini isiendelee kututafuna na kuturudisha nyuma. Tufunguke kifikra, tujenge mshikamano na umoja madhubuti. Tufanye kazi kwa bidii na kutumia fursa zilizopo katika kujiajiri. Zaidi sana tujenge Africa bora, jasiri na madhubuti yenye kulinda rasilimali zake kwa manufaa ya watu wake.
Tuwe na sauti moja Africa tuupinge ukoloni mamboleo, historia isijirudie, kila mmoja anajukumu la kuijenga Africa mathubuti,. Marais wa Africa tarehe 10/10/2013 muwe na sauti moja mathubuti yenye tija kwa Africa. Msiogope ijengeni historia mpya Afrika. Pamoja tuijenge Afrika madhubuti.
             Imeandikwa na Faraja Simon
            Email: farajasimon@yahoo.com, farajasimonm@gmail.com

            mobile: +255787539392, +255763222443

Tuesday, March 25, 2014

NIMEONA LEO TUTAFAKARI MANENO HAYA YA MWALIMU YANAYOISHI.

Mwalimu Julius K Nyerere



Na Faraja Simon
Uchaguzi wa mwaka mkuu umekaribi, bali tutaanza na uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa.Nimejaribu kufikiri dhana pana ya uongozi katika taifa hili.Nimefikiri juu ya utayari wa viongozi wetu kutatua matatizo tuliyonayo kama wananchi, si utayari tu pia na uwezo wao katika katika dhana ya uwajibikaji.
Wengi wa viongozi wetu wapo tayari waongoze mpaka wanakufa, wanasahau kuwa uongozi ni dhamana anapewa na wananchi kwa muda maalum. Anasahau kuwa kuna wengine wenye uwezo wa kushika nafasi hizo na kuleta fikra mpya na mabadiliko kuendana na uhitaji wa taifa na wananchi kwa ujumla wake. Wako tayari kuibaka demokrasia ili wabaki madarakani kwa kutumia esa kama silaha ya kuendelea kutawala.Hili nimeliona sana kwa wabunge na madiwani.Nikaona si vibaya tukijikumbusha maneno haya ya mwalimu nyerere. Aliyoyasema ni dhahiri kuwa yanatokea sasa. Mwalimu alisema:


"Plato, myunani wa kale, alipendekeza kuwa mafilosofa ndio wanaofaa kuwa watawala wa nchi, maana wana sifa mbili muhimu: Kwanza wana uwezo wa kutawala, na pili hawapendi kutawala. kwa hiyo jamhuri ya plato itakuwa na sheria ya kuwalazimisha mafilosofa kutawala kwa zamu; na mtu zamu yake ya kutawala ikiisha, atafurahi sana kurudia shughuli zake za falsafa ambazo ndizo hasa anazozipenda. lakini nchi zetu hazitawaliwi na mafilosofa wa plato; Watawala wetu ni wanasiasa wa kawaida ambao wanapenda sana kutawala, hata kama hawana uwezo wa kutawala; na ambao wako tayari hata kuhonga ili wachaguliwe kuwa watawala, na wakisha kuchaguliwa hawatoki bila kulazimishwa. " (uongozi wetu na hatima ya tanzania. zimbabwe publishing house, 1993: 8)


Toa maoni yako juu ya maneno haya ya mwalimu na mzalendo wa taifa letu.

TANZANIA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA



Na Faraja Simon
Tuwe makini na wanasiasa na tusiwaamini hata chembe hasahasa kwa hili la wao Kuhodhi mchakato wa uandishi wa katiba mpya.

Siasa ni sehemu ya maisha ya kila mtanzania hatuwezi kujitenga na siasa au siasa kutengwa nasi kwani imebeba mustakabali wa taifa letu.Pamoja na kuwa katiba ni political document , tuwe makini na siasa kuhodhi mchakato mzima wa bunge la katiba.Tusiruhusu wanasiasa kutufanyia maamuzi kwa madai kwamba ndio maamuzi ya watanzania zaidi ya milioni 44.Sio Madai na hoja zote za wanasiasa ni madai ya wananchi.N sio kweli kwamba wengi wao watasimamia na kutetea hoja za wananchi.

Wanasiasa watatafuta afueni ya vyama vyao hapo badae.Watawala wanatafuta katiba itakayotoa mwanya wa wao kuendelea kushika dola na wapinzania wanataka katiba itakayo wapa mwanya wa wao kushika dola kirahisi.Wanasiasa watatetea ugali wa watoto wao na nafasi zao hapo badae. Wengine wanatafuta ahuheni ya nafasi zao na za makundi yao hapo baadaye.Kwa hivyo ni wachache sana wanaofanya maamuzi yao kitaifa pasi na chembe za uchama.

Tusisahau kuwa uzalendo kwa wanasiasa wetu si wa kuridhisha, namaanisha ubinafsi umetawala fikra zaoWengi wao ni wachumia tumbo ,tusipokuwa makini watatuharibia katiba yetu kwa kuandika katiba yenye misingi na matakwa yao.Pamoja na kwamba tuna nafasi ya kuipigia kura ila tusisahau wanasiasa wana sauti ya kuwaaminisha watanzania visivyo vya kweli na kwa kuwaamini, tukawafuata.Hii itakuwa hatari kubwa kwa taifa letu.


Hatuna budi kuijenga,kuilinda na kuitetea Tanzania tunayoitaka. Ni Tanzania thabiti na yenye nguvu kubwa kiuchumi, kiusalama, siasa safi zenye lengo la kumkomboa mwananchi pale tu uzalendo utakapotunzwa kama lulu katika mioyo ya watanzania, pale rushwa atakapokuwa adui wa kila mtanzania, na Pale viongozi wa taifa hili watakapozika ubinafsi na kuishi uzalendo, kutetea rasilimali za taifa kwa manufaa ya taifa hili, wakiongoza mgawanyo sawa wa matunda ya rasilimali kwa taifa.


Tanzania inahitaji mabadiliko katika Nyanja zote.Hatuwezi kukataa mabadiliko au kuyapinga, tutayachelewesha tu.Tanzania inahitaji viongozi watendaji na sio waongeaji,watakaothubutu kuwa chachu ya mabadiliko chanya katika nyanja zote za maisha ya Mtanzania. Viongozi wenye maamuzi ya kizalendo kwa manufaa ya watanzania.Maamuzi wanayoyafanya au waliyowahi kuyafanya viongozi wetu kwa maslahi yao binafsi au ya mrengo wao yamelitafuna taifa na kuliweka hapa lilipo, yamepoteza dira ya Tanzania kama taifa.


Naamini Tanzania tunayoitaka ipo na itakuwa.Vijana tunaweza kuweka pembeni itikadi za kisiasa na kidini, ukabila, na ubinafsi.Na kuuvaa uzalendo na spirit ya kufanya kazi kwa bidii,kuichukia rushwa kwa moyo wetu wote,  kuwa watendaji zaidi ya waongeaji kwa manufaa ya Tanzania yetu. Tusiseme "walikula sasa zamu yetu".Bali tupatapo nafasi twende tukafanye kazi ya kuwatumikia watanzania kwa uaminifu na uzalendo wa hali ya juu.Tuwe na fikra za mabadiliko kwani naamini ipo siku vijana tutaandika historia mpya kwa taifa hili.


Na Faraja simon