AFRICA NA
UKOLONI MAMBO LEO NA ICC: KWANINI AFRICA?
Maisha ya binadamu hayajawahi kuwa maraisi au mepesi. Kila mmoja
hupambana ili kuweza kuyamudu. Kuna njia nyingi za kupambana ila moja kubwa
inayotumiwa na mabepari (capitalist) ni
kunyonya mataifa dhaifu (maskini). Hutumika kila njia ikiwezekana kuhatarisha
maisha ya maskini ili kujinufaisha. Utu kwa bepari ni nadharia tu. Kwani
hutunga chochote kile kulinda nafsi yake (status) katika Dunia.
Waliamua kuitawala
Africa ili kuweza kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyao pamoja na soko la
bidhaa zao kutokana na ushindani uliokuwepo. Hapa walikuja kama wamisionari,
wafanyabiahsara na wanajiografia. Hayo yote yalikuwa ni mwamvuli tu. Bali lengo
kuu ni unyonyaji wa nguvu kazi ya Africa na rasilimali za Africa.
Waafrica wenzangu,
tutambue ukoloni ulikufa na sasa wanatumia ukoloni mamboleo. Mimi huita
scientific colonialism, hutumia uwezo wao wa sayansi na teknolojia katika kutimiza
adhima yao ya kuzitumia rasilimali za
Africa na wanatumia njia zozote za kuvuna rasilimali hizi pasipo Africa
kujielewa. Kuna njia nyingi ila moja ni kuwathibiti viongozi hawa wa Africa
ambao wamekuwa wazalendo kwa Nchi zao na hawautaki ubeberu wao. Basi viongozi
hawa hudhibitiwa kwa njia mbili:
Moja ni kwa
mapinduzi ya waasi, hili mataifa haya huwafadhili waasi kwa siri sana, ili
kuziondoa serikali hatarishi uongozini wapate upenyo wa kuendeleza unyonyaji (Divide
and rule).
Pili ni hii
mahakama ya ICC (The Hague). Hutumia mahakama hii kama fimbo ya kuwaadabisha
viongozi wa kiafrica. Rais wa Libya asingekufa angekuwa the Hague, vivyovivyo
kwa Misri, Sudan na sasa ni Kenya. Africa lazima tuungane katika hili kwani leo
ni Kenya kesho Uganda, Tanzania, Malawi na hata Africa kusini pale tutakapokuwa
ukuta kuzuia unyonyaji wao.
Ndipo swali hili linakuja
kwa nini Africa? Ni swali kila mzalendo wa Africa atajiuliza, kwa nini Afrika!
Na sio Ulaya, Amerika, Australia na Asia? Je, umoja wa mataifa ni kwa ajili ya
Afrika pekee?
Ijumaa ya tarehe
10/10/2013 Nchi wanachama wa umoja wa Africa watakutana mjini Addis Ababa mada
kuu ikiwa ni mahusiano ya Africa na ICC. Shukran kwa Kaguta Yoweri Museven. Suala
hili linaumiza kichwa diplomasia ya Ulaya na America huku ikiwa kama panaweza
kutokea shinikizo la Nchi wanachama wa umoja wa Africa kujitoa katika mkataba
wa Rome.
Waafrica wenzangu,
ni lazima tujiulize maswali juu ya uwepo wa ICC na utendaji wake ndani ya
Africa. Kwanini ni viongozi wa kiafrica tu ndio wanao kwenda The Hague? Je!
Wanataka kutuambia kuwa mataifa ya
Magharibi hawakiuki haki za binadamu? Tujiulize kuhusu alichokifanya George W.
Bush kule Iraq na Pakistan, walichokifanya umoja wa Ulaya na Marekani(Obama)
kule Libya. Je, hii haitoshi kuwashitaki nao wakaenda The Hague? Kwa nini
Afrika?
Wafrika wenzangu, tumekuwa
wanyonge sana na tumekosa umoja ya kusema sasa inatosha kwa udhalimu huu wa
ICC. Tafadhali viongozi wan chi wanachama wa umoja wa Afrika mkutanapo tar
10/10/2013 muwe na sauti moja yenye maamuzi magumu itakayoitikisa Dunia na
kuifikishia ujumbe kuwa udhalimu na unyonyaji huu umetosha, umefika kikomo
Nionavyo ni vyema
umoja wa Africa ukawa na mahakama yake ili kuweza kuyamaliza mambo ya ndani ya
Africa, kwani tuna tamaduni zetu za kumaliza mizozo, na tuna tamaduni zetu za
kusuluhishana. Haina haja ya ICC kuendeleza udhalimu huu Afrika. Tuungane
pamoja katika maamuzi ya kujenga Africa madhubuti.
Sio hivyo tu, bali
najiuliza pia mahakama hii ilianzishwa kwa misingi gani? Nani walikuwa
walengwa? Kuna nini nyuma ya mahakama hii? Tuangalie zaidi ya kikomo cha macho
yetu yaonapo. Naamini kwa mwendo wa ICC, basi ni dhahiri kuwa ni fimbo ya kuiongoza
Africa katika kuimarisha na kusimika mizizi ya ubepari Africa.
Tumewahi kujiuliza
ni nani anayewafadhili waasi Africa? Je ni kweli huitaji kuingia madarakani kwa
demokrasia tena walioileta wao wenyewe ? wao wenyewe tena husaidia waasi
kuingia madarakani? Ni dhahiri kuwa kuna tusichokiona hapa. Nani
anayegharamikia silaha wanazotumia waasi?, ni nani aliyenyuma yao? Kwa mfano wa
Libya, ni nani aliyewaandaa waasi katika kumwangusha simba wa Africa aliyekuwa
adui mkubwa wa Amerika? Lazima tukubali
yaliyotokea Libya haikuwa ridhaa ya wanalibya bali kuna siri nzito nyuma yake. Kwanini
Afrika?
Waafrica wenzangu
haya yote yanayofanyika na wabepari hatuyaoni? Kwa nini tuwahukumu waafrica
wenzetu? Kwa nini tutumike kama chombo cha kuiangamiza Africa yetu kwa faida ya
wabepari? Kwa nini tufanywe wajinga na wavivu wa kufikiri kiasi hicho. Tuseme
imetosha, pamoja tujenge Africa mathubuti.
Mazingira ya machafuko ya kisiasa Afrika huziandaa wenyewe kwa
agenda zao za siri kisha wanakuja kutuadhibu na chombo hichi, mahakama ya
ICC.Nataka tuelewe kuwa mbali na mahakama hii viongozi wengi wa Africa huwekwa
madarakani wakiwa wameandaliwa kutimiza matakwa ya mabepari. Viongozi wengi wa
Africa ni mapandikizi ya mabepari yanayoiangamiza Africa yao wenyewe ndio maana
hawana maamuzi ya umoja.
Funguka Africa, ICC ni kiini macho tu, kuna mengi nyuma ya pazia. Tuukatae
ukoloni mamboleo ulioshika mizizi. Tuwe wamoja kujenga Africa mathubuti,
tusipigane wenyewe kwa wenyewe, tukatae kuwa mashabiki wa magharibi. Tujifunze
kwa Libya walivyoishabikia America, Nato na waasi pasipo kujua kuwa
wanajiangamiza wenyewe. Je divide and rule haijatunga kazi kule Libya? Marekani
alichukua tani ngapi za matuta? Fikiri kwa nini Afrika?
Waafrica wenzangu, tuache ushabiki wa kisiasa ulio na hisia za
kipandikizi pasipo kujijua, tutaiangamiza Africa sisi wenyewe.Historia
imetuweka tulipo lakini isiendelee kututafuna na kuturudisha nyuma. Tufunguke
kifikra, tujenge mshikamano na umoja madhubuti. Tufanye kazi kwa bidii na
kutumia fursa zilizopo katika kujiajiri. Zaidi sana tujenge Africa bora, jasiri
na madhubuti yenye kulinda rasilimali zake kwa manufaa ya watu wake.
Tuwe na sauti moja Africa tuupinge ukoloni mamboleo, historia
isijirudie, kila mmoja anajukumu la kuijenga Africa mathubuti,. Marais wa
Africa tarehe 10/10/2013 muwe na sauti moja mathubuti yenye tija kwa Africa.
Msiogope ijengeni historia mpya Afrika. Pamoja tuijenge Afrika madhubuti.
Imeandikwa na Faraja Simon
mobile:
+255787539392, +255763222443
0 comments:
POST A COMMENT