AFRIKA TUNA CHA KUJIFUNZA KWA UONGOZI WA RAIS KENYATTA NA JUHUDI ZAKE ZA KUIKOMBOA AFRIKA KIUCHUMI. | Gossip Wire
Breaking News
Loading...

Sunday, May 11, 2014

AFRIKA TUNA CHA KUJIFUNZA KWA UONGOZI WA RAIS KENYATTA NA JUHUDI ZAKE ZA KUIKOMBOA AFRIKA KIUCHUMI.

Na Faraja Simon
Pongezi zangu kwa rais wa Kenya kwa kuonyesha uwazi hasa kwa kuweka mkataba waliokubaliana na serikali ya uchina wazi. Sio kitu rahisi hata kidogo kwa mataifa ya afrika kufanya kitendo hicho. Ameweka wazi kupitia ukurasa wake wa facebook. kuisoma fuata link hii UHURU KENYATTA.



Kijana huyu amekuwa mstari wa mbele kutetea na kuonyesha nja kwa afrika kukuza pato la ndani kwa kufungua milango ya biashara kati ya nchi moja ya afrika kwenda nyingine.Hapa juzi kwenye world economic forum alikuwa na ajenda hiyohiyo ya kuongeza masoko ya ndani na free movement of goods.Kuwapa nafasi wawekezaji wa ndani kuwekeza ndani ya Afrika. Kuondoa vizuizi vya kibiashara na mengineyo.Haya ni maneno yake aliyoandika may 7 2014 kupitia ukurasa wake wa Facebook:
"Today during the World Economic Forum onAfrica, I called on all African leaders to work together in removing obstacles that hinder movement across the continent. Free movement of people, goods and services will increase intra-Africa trade and help the continent achieve its development targets. Lack of political will and negative perception should not be allowed to undermine Africa’s integration and economic growth. As leaders, we should not block African investors from investing in the continent by imposing stiff regulations and cumbersome visa requirements. We need to facilitate our business people to trade within the continent more freely. There is no reason why we cannot begin by issuing proven African investors with visas allowing them to do their work with minimum of difficulties. We signed the call to action by the World Economic Forum’s Global Agenda Council on Travel and Tourism."

Kijana huyu ana kitu cha tofauti bado hakijaonekana ila naamini ipo siku kitaonekana. Afrika izidi kumpa nafasi na kummunga mkono katika kuikomboa Afrika kiuchumi.

Kaonyesha njia kwa wana Afrika na Afrika mashariki kwa ujumla na ni nafasi kwa Tanzania kujifunza kupitia hilo. Mh: JK mikataba mnayotia sahihi iwekeni wazi tuione. Mnaficha nini ingali taifa ni la watanzania tupeni nafasi ya kuona makubaliano yenu.

Najua unatangaza uwazi kwa serikali yako, ila mkuu wangu wa nchi jaribu kuwa muwazi kwenye serikali yako. Uwazi ni pamoja na mikataba hiyo kuwa wazi. Demokrasia ni pamoja na mikataba hiyo kuwa wazi. Embu angalia hili suala mkuu na jua lipo ndani ya uwezo wako.

-F.S

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT